Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_2e4e1029dca1e09ab543322328909931, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Mapishi ya Biriani
Date: April 9, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Mahitaji
Mchele (rice 1/2 kilo)
Nyama (beef 1/2 kilo)
Vitunguu (onion 2)
Kitunguu swaum (garlic 1 kijiko cha chai)
Tangawizi (ginger 1 kijiko cha chai)
Maziwa mgando (yogurt 1 kikombe cha chai)
Hiliki nzima (cardamon 6)
Amdalasini nzima (cinamon stick 2)
Karafuu nzima (cloves 6)
Pilipili mtama nzima (black pepper 8)
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Binzari manjano (turmaric 1/2 kijiko cha chai)
Binzari nyembamba nzima (cumin 1/4 kijiko cha chai)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia nyama na uikaange kwa muda wa dakika 10. baada ya hapo tia tangawizi, kitunguu swaum, hiliki(4), amdalasini (1), karafuu (4), pilipili mtama (5), Curry powder, binzari manjano, binzari nyembamba na chumvi. Kisha koroga. Baada ya hapo tia yogurt na uipike mpaka ikauke kisha tia maji kidogo, funika na upunguze moto na uache ichemke kwa muda wa nusu saa.Baada ya hapo nyama itakuwa imeiva na mchuzi kubakia kidogo.Kwahiyo itatakiwa kuiipua.
Loweka mchele kwa dakika 10. kisha chemsha maji mengi kidogo katika sufuria kubwa. baada ya hapo tia hiliki (2) amdalamsini (1) karafuu(2) pilipili mtama (3) chumvi na mafuta kiasi. acha ichemke kidogo kisha tia mchele.Hakikisha maji yameufunika mchele kabisa na uuache uchemke kwa muda wa dakika 8 tu (kwani hautakiwi kuiva kabisa) kisha uipue na uchuje maji yote katika chujio. baada ya hapo chukua sufuria ya kuokea (baking pot kama unayoiona kweye picha) Kisha weka wali nusu na uusambaze sawia kisha weka mchuzi nyama na mchuzi wake pia utandaze na umalizie kwa kuweka leya ya wali uliobakia. Baada ya hapo ufunike na uweke kwenye oven kwenye moto wa 200°C kwa muda wa nusu saa.na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_2e4e1029dca1e09ab543322328909931, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Mahitaji
Viazi ulaya (baking potato 5 vya wastani)
Parprika 1 kijiko cha chai
P...
Read More
Viamba upishi
Mgagani mkono 1
Mafuta vijiko vikubwa 4
Karanga zilizosagwa kikom...
Read More
Mahitaji
Maharage yaliyochemshwa kiasi
Spinach zilizokatwa kiasi
Vitunguu maji ...
Read More
• Kula chakula bora kunamaanisha kula vyakula aina tofauti ya vyakula kila siku kama vile matun...
Read More
Mahitaji
Mchele - 2 vikombe
Adesi -1 ½ vikombe
Nazi ya unga - 1 Kikombe
<...
Read More
Upishi wa Afya kwa Kompyuta: Milo Rahisi na yenye Ladha 🍲🖥️
Hivi leo, AckySHINE an...
Read More
MAHITAJI
Unga kikombe 1 ½
Siagi ½ kikombe
Sukari ½ kikombe
Yai 1
...
Read More
MAHITAJI
1 kilo unga wa ngano
240 ml maji ya vugu vugu
2 olive oil kijiko kikub...
Read More
Viamba upishi
Unga
2 Magi (kikombe kibuwa cha chai)
Sukari
1/3 Kikombe ch...
Read More
Mahitaji
Viazi (potato) 1 kilo
Nyama ya ng'ombe 1/2 kilo
Nyanya ya kopo iliyosa...
Read More
Mahitaji
Mchele wa Par boiled au basmati - 5 vikombe
Nyama kondoo/mbuzi ya kusaga -...
Read More
Mahitaji
Mchele wa basmati - 3 vikombe
Kuku - ½
Viazi - 4
Vitunguu - 2...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!