Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/right_sidebar.php on line 13

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/right_sidebar.php on line 13
Sidebar with Floating Button
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 3

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 14

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 14
MHUBIRI
☰
AckyShine
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line 4

Chanzo, dalili, aina na matibabu ya ugonjwa wa kifafa

Featured Image
Huu ni ugonjwa ambao unasabababishwa na seli zilizopo katika mishipa ya fahamu zilizopo kwenye ubongo kutoa umeme[impulses] mwingi kuliko kawaida kwenda kwenye misuli na sehemu zingine za mwili, na kusababisha mtu kupata dalili kama vile kuishiwa nguvu, kichwa kuuma, kuchanganyikiwa, mwili kukakamaa na hata kupoteza fahamu. Hali hii hujirudia mara kwa mara.

Ifahamike kuwa, aina ya kifafa inayojulikana sana mitaani ni ile ambayo mtu anakakamaa na kupoteza fahamu, japokuwa kuna aina za kifafa ambazo mtu hakakamai wala kupoteza fahamu, kama tutakavyoona hapo baadae.

Mwaka 2013 ugonjwa huu uliua zaidi ya watu laki moja duniani, 80% wakiwa waafrika.

Mgonjwa huyu huweza kuanguka mara kadhaa kwa mwezi lakini anaweza asianguke kabisa kama anafuata masharti na utaratibu mzuri wa matibabu…

Chanzo cha ugonjwa wa kifafa ni nini?


Chanzo kikuu cha ugonjwa huu kwa watu wengi hua hakifahamiki lakini baadhi ya hiz ni moja ya sababu za kuugua kifafa.

Kurithi; familia na koo zingine zinakua na ugonjwa huu hivyo watoto na wajukuu huzaliwa tayari na ugonjwa huu.

Kuumia kichwa: ajali zinazohusisha kuumia kwa kichwa huweza kusababisha kuumia kwa mishipa ya fahamu na mtu kuugua kifafa.

Magonjwa mengine; kuna magonjwa mtu akiugua maishani mwake baadae huweza kupata kifafa kwasababu magonjwa hayo yanavyoharibu mfumo wa ubongo.. mfano homa ya uti wa mgongo kitaalamu kama meningitis.

Uvimbe kwenye ubongo: matatizo ya uvimbe kwenye ubongo kama kansa huweza kusababisha mtu kuugua kifafa.

Kiharusi; huu ni ugonjwa ambao husababishwa na damu kushindwa kupita vizuri kwenye ubongo au kupasuka kwa mishipa ya damu ya ubongo hali hii husababisha mtu kupooza nusu ya mwili wake na huweza kuugua kifafa baadae.

Matatizo wakati wa kuzaliwa: wakati mwingine mtoto huzaliwa kwa shida sana kwa njia ya kawaida kiasi kwamba kichwa chake hubanwa sana wakati wa kupita na hali hii huweza kumsababishia kifafa kwanzia utotoni.

Matatizo ya utengenezaji wa mtoto tumboni; wakati mwingine ile miezi mitatu ya kwanza ambayo mtoto ndio anapata viungo tumboni huweza kutokea kasoro kwenye mfumo wa fahamu za kwenye ubongo na kumfanya apate kifafa akizaliwa.

Magonjwa ya uzee yanayoathiri ubongo; kuna magonjwa huharibu ubongo wakati wa uzee na magonjwa haya huweza kusababisha kifafa kipindi hicho.

Aina za kifafa


Kuna aina mbili kubwa za kifafa:

1)Primary marygeneralized seizures


Hii ndio aina ya kifafa ambayo inafahamika sana mitaani; na inahusisha mgonjwa kukamaa, na kupoteza fahamu, pamoja na dalili zingine kama vile kutoa povu mdomoni, na kujisaidia haja kubwa na/au ndogo bila kujitambua akishikwa na hali hiyo.

Pia wengine hupatwa kama na wazimu au kuchanganyikiwa kwa muda kabla au baada ya kushikwa na hali hiyo.

2)Partial seizures


Aina hii ya kifafa ni ile ambayo haihusishi muhusika kupoteza fahamu na kukakamaa!! Bali hushikwa na hali fulani kama ya bumbuwazi kwa dakika kadhaa; Wengine huwa na dalili zisizoeleweka za mara kwa mara kama vile kusihiwa nguvu, kizungu zungu, kichwa kuuma sana (bila sababu ya kiafya inayojulikana), na kadhalika. Aina hizi za kifafa ziko nyingi, na dalili hutofautiana kwa kadri ya aina ya kifafa!!

Vipimo vinavyofanyika kugundua kifafa


Ugonjwa huu unaweza kutambulika kwa daktari kuchukua historia ya dalili zinazomkabili muhusika tu(hakuna kipimo ambacho kinaweza kutambua kifafa kwa asilimia 100); Kuna kipimo kinachopima jinsi ubongo unavyotoa taarifa za umeme (ELECTROENCEPHALOGRAM-EEG), ambacho kinaweza kutambua kifafa, lakini kipimo hiki kinaweza kikaonekana kuwa hakina shida, na bado mtu akawa na tatizo hilo la kifafa. Hivyo basi, kifafa ni moja kati ya magonjwa machache ambayo kutambulika kwake kunategemea sana ujuzi na utaalamu wa daktari katika kuunganisha dalili za mgonjwa kuliko vipimo!!

Hata hivyo, mara nyingi nyingi mgonjwa hupimwa vipimo tofauti ili kuweza kujua chanzo cha ugonjwa… mfano

β€’ Uwezo wa kufanya kazi figo

β€’ Uwezo wa kufanya kazi maini

β€’ Kupima maji ya uti wa mgongo

β€’ Kupima Kaswende

β€’ Picha ya ubongo mfano CT SCAN.

Mambo yanayofanya kupata degedege za kifafa mara kwa mara..

β€’ Kukosa usingizi kwa muda mrefu

β€’ Mianga na miale ya disko

β€’ Unywaji wa pombe

β€’ Kuishiwa sukari mwilini wakati wa akisikia njaa kali.

β€’ Kutomeza dawa kama ilivyoelekezwa

Huduma


Matibabu yasiyo ya dawa wakati mgonjwa amekamatwa na kifafa:{non pharmacological treatment}yaani HUDUMA YA KWANZA

β€’ Mzuie mgonjwa asijiumize kwa kuweka kitu laini chini ya kichwa chake, ondoa vitu vikali karibu yake kama kisu, sindano au vyuma.

β€’ Usilazimishe kitu chochote kwenye mdomo wa mgonjwa.

β€’ Usimshike kuzuia mizunguko yake

β€’ Weka kichwa alale anaangalia upande mmoja ili kutoa mate mdomoni.

β€’ Kaa na mgonjwa mpaka degedege ziishe

β€’ Usiweke chochote mdomoni kwa mgonjwa kama dawa au chakula mpaka apate fahamu zake.

Mtu mwenye kifafa hali hii ya kukamatwa na degedege za kifafa sio ya ajabu sana ila ukiona dalili hizi mkimbize hospitali..

β€’ Degedege za kifafa zaidi ya dakika kumi

β€’ Kutapika sana

β€’ Kushindwa kuona vizuri

β€’ Kupoteza fahamu

β€’ Kichwa kuuma sana.

MATIBABU YA UGONJWA


Kama kawaida chanzo cha ugonjwa kikipatikana mgonjwa huanzishiwa matibabu lakini kama mgonjwa alikua tayari ameshapata madhara kwenye ubongo kulingana na chanzo husika ataendelea kua na kifafa.

Ugonjwa wa kifafa hauponi kabisa kwa 100% hospitali, ukishaambiwa una kifafa au mgonjwa wako ana kifafa basi utapewa utaratibu wa matibabu yaani kumeza dawa siku zote za maisha yako na kufuata baadhi ya masharti na utaishi maisha ya kawaida kabisa.
AckySHINE Solutions

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line 4

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Dondoo muhimu kwa Afya yako unapostuka usiku

Dondoo muhimu kwa Afya yako unapostuka usiku

Kumekuwepo na tatizo la vifo vya ghafla sana tena kwa watu ambao wana afya njema na hii inatokana... Read More

Tiba kwa kutumia maji

Tiba kwa kutumia maji

β­•Tiba kwa kutumia majiβ­•
πŸ’§πŸ’§πŸ’§πŸ’§πŸ’§πŸ’§πŸ’§πŸ’§πŸ’§

Hamuwezi kuamini! mar... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia baking soda

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia baking soda

Moja ya sababu za kutokea chunusi katika ngozi yako ni kuwepo kwa takataka au uchafu juu ya ngozi... Read More

Unachotakiwa kujua kuhusu Shinikizo la chini la damu

Unachotakiwa kujua kuhusu Shinikizo la chini la damu

Ugonjwa wa Shinikizo la chini la damu ambao hujulikana kama hypotension kwa Kiingereza ni hali am... Read More

Madhara ya kuwa mnene kupindukia

Madhara ya kuwa mnene kupindukia

Unene(obesity), ni ugonjwa unaokua kwa kasi kipindi hiki ukiambatana na madhara makubwa kiafya hata ... Read More
Faida 10 za kulala mapema kiafya

Faida 10 za kulala mapema kiafya

Mapera ni matunda yanayo patikana kwa wingi lakini mara nyingi huwa hayapendelewi sana kutokana n... Read More

Matumizi ya tunda la shelisheli kama dawa ya ngozi

Matumizi ya tunda la shelisheli kama dawa ya ngozi

Shelisheli lililokomaa huwa na uzito wa hadi kilo 6, ambapo mshelisheli unaweza kukua kwa urefu w... Read More

Dondoo Muhimu kuhusu ugonjwa wa kisukari

Dondoo Muhimu kuhusu ugonjwa wa kisukari

Wapendwa, napenda kushirikiana na nyinyi kujuzana hili nililolisikia kupitia channel ten leo asub... Read More

Mambo 9 ya kuzingatia kuepuka ugonjwa wa saratani au Kansa

Mambo 9 ya kuzingatia kuepuka ugonjwa wa saratani au Kansa

Tafiti nyingi zilizolizofanywa zinaonesha kuwa sababu kuu zinazosababisha saratani ni mtindo wa mais... Read More
Vyakula vinavyoongoza kuongeza akili kwenye ubongo

Vyakula vinavyoongoza kuongeza akili kwenye ubongo

BILA shaka ubongo ni miongoni mwa viungo muhimu vya binadamu lakini ni watu wachache sana wanaout... Read More

Namna ya kutibu chunusi kwa kutumia asprin

Namna ya kutibu chunusi kwa kutumia asprin

Aspirin inaweza kuwa ni moja ya dawa nzuri za chunusi. Chukua vidonge viwili au vitatu vya aspir... Read More

Magonjwa hatari 10 yanayotibika kwa kutumia mbegu za Maboga

Magonjwa hatari 10 yanayotibika kwa kutumia mbegu za Maboga

Mbegu za maboga zina protini na madini ya kutosha na ya mhimu zaidi mwilini kama madini ya zinki,... Read More


Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e512tcknrfclmbq5m4qr0l94qc, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/bottom_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/bottom_menu.php on line 3
πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact