Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_1ae19c5bf2d0e0de5e2fa13cc6b53ce3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Faida 25 za kutembea kwa Miguu
Date: April 15, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo.
Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii.
Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida za kutembea kwa miguu.
- Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu.
- Huimarisha mifupa.
- Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi.
- Husaidia kupunguza uzito.
- Huzuia saratani ya utumbo mpana.
- Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua.
- Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance).
- Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya mazoezi yanayoleta uwiano wa urefu na uzito β BMI; jambo litakalokukinga na aina ya pili ya kisukari (Type 2 Diabets).
- Hukabili shinikizo la damu.
- Huondoa msongo wa mawazo.
- Huongeza utayari.
- Hukufanya ujifunze mambo mbalimbali kwa kuona.
- Hukuokolea gharama za nauli au mafuta.
- Hupunguza lehemu mbaya mwilini (cholesterol)
- Huimarisha misuli.
- Husaidia mmengβenyo wa chakula kwenda vizuri.
- Huwezesha kinga mwili kujiimarisha na kujijenga (kutokana na sababu kuwa kutembea ni aina ya zoezi).
- Huboresha uwezo wa kumbukumbu.
- Hukujengea mahusiano ya kijamii. Unapotembea utakutana na watu mbalimbali.
- Huzuia kuzeeka. Utafiti uliofanyika ulibaini kuwa watu wanaotembea umbali mrefu huishi zaidi.
- Hukuweka katika hali nzuri (mood).
- Hukusaidia kulala vizuri. Kumbuka mazoezi ni chanzo cha usingizi mzuri.
- Huboresha afya ya uzazi hasa kwa wanaume. Kutembea kama zoezi ni njia ya kuwapa wanaume nguvu katika afya ya uzazi.
- Huzuia kuharibika kwa mimba. Mazoezi ni muhimu sana kwa mama mjamzito kwa ajili ya afya yake na mtoto; hivyo zoezi rahisi na jepesi kwake ni kutembea.
- Huboresha mwonekano wa mwili. Mazoezi ni njia moja wapo ya kuufanya mwili wako uonekane katika umbo zuri. Hivyo kutembea kama aina mojawapo ya zoezi kunaweza kukusaidia sana.
Naamini umeona jinsi ambavyo kutembea kwa miguu kuna manufaa makubwa sana kwenye afya, uchumi na hata mahusiano yako ya kijamii.
Inashauriwa kuhakikisha unatembea kwa miguu angalau dakika 30 kila siku. Kwa njia hii utapata manufaa mengi yaliyotajwa hapo juu.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_1ae19c5bf2d0e0de5e2fa13cc6b53ce3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Unaweza kutumia Lozi na maziwa kutibu shinikizo la chini la damu kama ifuatavyo;
- Lowek...
Read More
Mbaazi ni zao la chakula ambalo linalimwa sehemu nyingi sana hapa nchini, zao hili pia linaweza k...
Read More
Upungufu wa damu ni tatizo linalosababishwa na kupoteza damu nyingi, kupungua kwa uzalishaji wa chem...
Read More
Harafu ya jasho inakera, kibaya zaidi ni kuwa wewe mwenyewe husikii harufu hiyo ila wale walio ka...
Read More
Hatua za kufuata
1. Tengeneza glasi moja ya juisi ya karoti
Peasi ni tunda ambalo limekuwa halithaminiwi licha ya kuwa na faida lukuki katika mwili wa binada...
Read More
Mbegu za maboga zina protini na madini ya kutosha na ya mhimu zaidi mwilini kama madini ya zinki,...
Read More
ββpiga chini kitambiββ
Mahitaji
πΉTikitiπ 1
πΉTangawizi kid...
Read More
Kila mmoja wetu anaweza kuwa na sababu tofauti inayoweza kumsababishia msongo (stress). Sababu ku...
Read More
Hii inaweza kuchukuliwa kama njia rahisi na isiyo na gharma katika kutibu chunusi. Kwa mjibu wa ...
Read More
Mchanganyiko wa mdalasini na asali ni dawa nzuri ya kutibu chunusi.
Changanya asali viji...
Read More
Siku zote sisi wanadamu huwa tunaambizana kuwa, kinga ni bora kuliko tiba, tukiwa na maana kwamba...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!