Log in to access your menu with tools for managing π tasks, π₯ clients, π° finances, π learning, π personal growth, and π spirituality, all in one place!.
Unganisha imani na maisha yako kupitia π Sala, π Masomo ya Misa, π Mafundisho, π‘ Tafakari, π° Makala, na π My System kwa usimamizi wa maisha binafsi. Tunakukaribisha kwenye safari ya kiroho na kimwili!.
Updated at: 2024-05-25 16:22:00 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndoto nyevu ni kitu kinachowatokea vijana wakiwa usingizini. Haiwezekani kuzuiwa kwa sababu uko usingizini, lakini labda ingekuwa vizuri wewe kujiuliza kwa nini unataka kuzuia jambo hili, haswa ukizingatia kwamba ndoto nyevu hazidhuru afya yako kabisa na kwamba ni dalili kuwa sasa unakuwa mtu mzima, yaani mwanaume.
Je, kuna madhara msichana akifanya mapenzi wakati akiwa katika hedhi (siku zake)?
Updated at: 2024-05-25 16:22:09 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kufanya mapenzi wakati msichana yuko katika hedhi hakuna madhara yoyote kiafya kwa mwanaume wala mwanamke kama kati yao hakuna mwenye ugonjwa wa zinaa.
Ila kama mmoja wapo ana ugonjwa wa zinaa, huo ni wakati wa hatari sana kwa maambukizi, kwa sababu utando ndani ya mfuko wa uzazi unabomoka na mlango wa mfuko wa uzazi unakuwa wazi. Hivyo ni rahisi sana vijidudu vya magonjwa mbalimbali kuingia mwilini mwa msichana. Vilevile kama msichana tayari ameambukizwa na magonjwa ya zinaa, katika damu yake viko vijidudu vingi vinavyoweza kumwambukiza mvulana.
Kwa sababu mara nyingi ni vigumu kufahamu kama kati ya wapenzi hakuna mwenye ugonjwa wa zinaa, haishauriwi kujamii ana wakati wa hedhi na kama ndivyo basi kondomu i tumike.
Katika jamii nyingi kujamii ana wakati mwanamke yuko wenye hedhi haikubaliki kwa sababu ya mila au dini.
Updated at: 2024-05-25 16:22:41 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Tunaposema dawa za kulevya ina maana ni matumizi mabaya ya dawa na hasa pale yatumikapo kinyume cha maelekezo ya tabibu na hivyo kuleta madhara kwa mtumiaji.
Ni hatua gani zinazochukuliwa na serikali ili kukomesha vitendo vya kuwinda Albino?
Updated at: 2024-05-25 16:24:12 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kufuatia vitendo vibaya vya mauaji ya Albino, vilivyozuka Tanzania tangu mwaka 2007 hadi sasa, Serikali imechukua hatua kadhaa kurekebisha hali hiyo. Hatua hizo ni pamoja na: β’ Kuliagiza jeshi la polisi kuwatafyta na kuwakamata wauaji wa aalbino. β’ Kumteua Albino kuwa Mbunge wa Viti Maalumu Wanawake. β’ Kutangaza hadharani kuwa mauaji haya siyo utamaduni β’ bali ni uhalifu mbaya ambao lazima uchukuliwe hatua za kisheria. β’ Kutaka mikoa yote watangaze majina ya watu wote wanahusika na mauaji haya. β’ Kuliagiza jeshi la polisi kuwatafuta na kuwakamata wauaji wa Albino. β’ Kuanzishwa kamati maalumu ya mahakimu ili kuharakisha hukumu za wauaji. β’ Viongozi wa juu wote wanalaani vitendo hivi katika mikutano ya hadhara na matukio maalumu kama wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2009.
Iwapo mtu mzima amejamiiana na mtoto na wote wawili wamekubaliana
Updated at: 2024-05-25 16:24:02 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ni kweli hiyo ni dhuluma na inaitwa unyanyasaji wa kijinsia kwa mtoto. Watoto wanaweza kushawishiwa kwa kutumia hila kwa mtu mzima anayejaribu kuwavuta ili waweze kujamiiana naye. Na zaidi wanaweza wasielewe matatizo au madhara watakayopata kutokana na kujamiiana kwa afya zao pia wanaweza wasiweze kufanya maamuzi sahihi kwa vile hawana habari. Mtoto hana uwezo wa kuchunguza mambo katika akili yake kabla ya kujamiiana. Uhusiano unaweza pia usiwe sawa kwa vile yule mtu mzima ana uwezo na nguvu juu ya yule mtoto. Kwa hiyo itakuwa vigumu kwa mtoto kujadiliana juu ya matumizi ya kondomu .Hizi ndiyo sababu kwa nini watoto wanahitaji ulinzi maalum. Ni kosa kujamiiana na msichana wa umri chini ya miaka 18. Iwapo mtu anajamiiana na msichana chini ya miaka 18 mtu huyo anawajibika kisheria, katenda kosa hata kama msichana amempa ridhaa yake.
Kuna athari gani za mimba za utotoni hasa kwa kijana Albino?
Updated at: 2024-05-25 16:24:09 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Katika masuala ya athari za mimba katika umri mdogo ni kwamba vijana Albino hawana tofauti na vijana wengine . Bado inashauriwa na kutiliwa mkazo umuhimu wa msichana kutopata mimba akiwa na umri chini ya miaka 18.
Sababu kubwa ikiwa ni kuwa mwili wa msichana ambaye umri wake ni chini ya miaka 18 haujakomaa vya kutosha kuweza kuhimili ujauzito bila matatizo. Katika umri huu mdogo, uwezekano mkubwa wa kupata matatizo yanayotokana na ujauzito, hasa wakati wa kujifungua. Uzoefu umeonyesha kuwa mara nyingi wakati wa kujifungua mtoto anashindwa kutoka na inabidi mama afanyiwe upasuaji. Pia katika umri huu uwezekano ni mkubwa mtoto kuzaliwa njiti (hajafikia muda wa kuzaliwa). Tatizo jingine linaweza kutokea pale ambapo kichwa cha mtoto ni kikubwa au mama anakuwa na uchungu wa muda mrefu na kusababishwa kuchanika kwenye mfumo wa uzazi kwenye njia ya haja ndogo au hata na njia ya haja kubwa na mama kupata fistula. Hali hii ikitokea itamfanya mama hatimaye awe anavuja ama haja ndogo au haja kubwa au vyote viwili kupitia njia ya ukeni.
Mbali na madhara haya ya kiafya, msichana anaweza kupata matatizo mengine ya kijamii kama vile kufukuzwa shule, kusababisha ugomvi ndani ya familia na jamii. Kwa mantiki hii, ni muhimu kwa vijana kusubiri hadi kufikia miaka 18 wakiwa tayari kuchukua / kubeba majukumu kama wazazi.
Updated at: 2024-05-25 16:22:40 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Moja kati ya vitu vinavyotisha kuhusu dawa za kulevya ni kwamba zinaathiri watu kwa njia mbalimbali na huwezi ukasema kwa uhakika jinsi zitakavyokuathiri. Madhara ya dawa za kulevya yanategemea aina, kiwango na jinsi zitakavyotumika. Vilevile inategemea na umri, afya ya mwili na ukomavu wa akili, na pia mazoea ya matumizi ya dawa hizo.
Madhara ya muda hutokea mara tu baada ya dawa za kulevya kutumika, wakati madhara ya muda mrefu huonekana baada ya muda kupita, na mara nyingi husababisha uharibifu wa kudumu kwenye mapafu na ubongo.
Kwa mfano, bangi, husababisha kuongezeka kwa mapigo ya moyo, matatizo ya kumbukumbu ya muda mfupi, pamoja na umakini, kujifunza, kufikiri na kutatua matatizo. Pia inaweza ikasababisha kasoro kwenye utaratibu wa viungo vya mwili. Mara kwa mara wavuta bangi huwa na macho mekundu. Na vijana wengine hupata mihemuko mbalimbali kama uoga na hofu baada ya matumizi ya bangi.
Dawa za kulevya za vichangamsho, kama mirungi na kokaini, inasemekana kuwa huwafanya watumiaji kuwa macho, kujiona wana nguvu na kujiamini. Vichangamsho vikitumika kwa wingi, humfanya mtumaji kujihisi kuwa na wasiwasi au hofu. Matumizi mabaya ya dawa za kulevya kwa muda mrefu huweza kusababisha matatizo ya akili au hata kifo i iwapo yatatumika kwa kiwango cha juu.
Dawa za kulevya zinazokufanya upooze kama heroini au dawa nyingine zinazoagizwa na daktari, husababisha kujisikia umetulia, una amani na furaha. Ukizidisha vipimo husababisha usingizi, upungufu wa umakini na uwezo wa kuona, kizunguzungu, kutapika na kutokwa jasho. Vilevile kipimo kingi kinaweza kusababisha usingizi wa muda mrefu, kuzimia na hata kifo.
Pombe za kienyeji kama gongo ni hatari kwa afya na zinaweza kusababisha upofu na hata kifo.
Matumizi ya dawa za kulevya hupunguza uwezo wa vijana kuhimili na kutatua matatizo yao ya kijamii na kiakili. Hii husababisha vijana kuwa wepesi kujihusisha na ujambazi na mambo ya ngono na ugomvi, mabadiliko hayo ya tabia husababisha ugomvi katika familia na kuvunjika kwa urafiki. Matumizi ya dawa za kulevya ndiyo sababu kubwa ya ajali za barabarani, kujiua na maambukizo mbalimbali.
Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?
Updated at: 2024-05-25 16:24:31 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Balehe ni kipindi cha mpito kati ya utoto na utu uzima, ambapo watoto wa kike na wa kiume wanapitia mabadiliko mbalimbali ya kimwili, kiakili, na kihisia. Kwa wasichana, mabadiliko haya yanaweza kujumuisha yafuatayo:
Ukuaji wa Viungo vya Uzazi: Ovari zinaanza kutengeneza mayai na homoni za kike kama estrogen na progesterone, ambazo husababisha mabadiliko mengine.
Hedhi (Menstruation): Wasichana wanaanza kupata hedhi, ambayo ni kumwagika kwa utando wa kizazi kila mwezi, isipokuwa kipindi cha ujauzito.
Ukuaji wa Matiti: Huanza kama vimbe vidogo chini ya chuchu na baadaye kukua zaidi.
Ongezeko la Urefu na Uzito: Kuna spurt ya ukuaji ambapo wasichana hukua haraka kwa urefu na kuongezeka uzito.
Mabadiliko ya Mwili: Mafuta ya mwili huongezeka hasa kwenye hips, makalio, na matiti, kusababisha umbo la mwili kubadilika na kuwa la kike zaidi.
Nywele za Mwili: Uotaji wa nywele katika sehemu za siri, kwapani, na nyakati nyingine kwenye mikono, miguu na uso.
Mabadiliko ya Ngozi: Ngozi inaweza kuwa yenye mafuta zaidi na kusababisha chunusi.
Mabadiliko ya Hisia na Tabia: Hisia zinaweza kubadilika haraka kutokana na mabadiliko ya homoni na mihadhara mingine ya kisaikolojia ya kipindi hiki.
Hizi ni baadhi tu ya mabadiliko yanayotokea wakati wa balehe kwa wasichana. Ni muhimu kuzungumza na watoto kuhusu mabadiliko haya na kuhakikisha wanapata usaidizi na taarifa sahihi kadri wanavyokua.
Kuna mabadiliko mengi ya kimwili ambayo yanatokea kwa msichana wakati anaingia utu uzima. Baadhi ya mabadiliko hayo ni kama yafuatayo:
Mabadiliko ya mwili
Kuongezeka urefu na kupanuka mwili haswa nyonga na matiti kuanza kukua;
Ngozi yako i taanza kuwa na mafuta mengi, unaweza pia kuota chunusi usoni;
Kuota nywele sehemu za siri (mavuzi) na makwapani; na
Kupata damu ya hedhi (kuvunja ungo).
Mabadiliko ya hisia
Kuanza kuwa na muhemko wa kutaka kujamii ana na wakati mwingine mwili wako unaweza kusisimka ukimwona mvulana anayekuvutia;
Mihemuko ya kupenda wanaume huongezeka na wewe kupenda kujipamba i li kuwa na mwonekano wa kupendeza; na
Kuanza kujiamini, kutotaka kulazimishwa kufanya baadhi ya vitu na wewe kutaka kuonekana kama mtu mzima anayeweza kufanya maamuzi pekee yake.
Mabadiliko haya ni jambo la kawaida kwa msichana balehe. Kumbuka, kila msichana anapitia mabadiliko haya katika nyakati tofauti na ukali / nguvu tofauti.
Je, zipo sheria zinazolinda watu wenye ulemavu hapa Tanzania?
Updated at: 2024-05-25 16:24:15 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ndiyo, zipo sheria hapa T a n z a n i a z i n a z o w a l i n d a watu wenye ulemavu. Tanzania ilitia saini na kuridhia mkataba wa kimataifa wa ulinzi, haki na usawa kwa watu wenye ulemavu mwaka 2006. Kwa kitendo hicho cha kuridhia mkataba huo wa kimataifa Tanzania imeonyesha nia yake ya kuwalinda na kudumisha haki za watu wenye ulemavu. Hata katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 19772 inakataza ubaguzi wa aina yoyote kwa watu wenye ulemavu. Zipo sheria nyingi zinazolinda haki na usawa kwa watu wenye ulemavu ambazo zinahusika na sekta mbalimbali. Kwa mfano; elimu na mafunzo, ajira3, matunzo4 na ustawi5 kwa ujumla. Ipo pia sera ya Taifa kuhusu ulemavu ya mwaka 20046. Sera hii imeweka mazingira muafaka kwa watu wenye ulemavu kupata haki sawa katika maendeleo ya kijamii, ikiwa ni pamoja na kupata huduma na mahitaji ya msingi kutoka katika jamii.
Sheria zinazolinda haki za Albino
Hakuna sheria mahususi inayowalenga watu wanaoishi na ualbino hapa Tanzaina. Ingawaje haki za msingi za Albino zinalindwa chini ya Katiba ya nchi pamoja na Sheria z i n a z o h u s i k a na sekta m b a l i m b a l i . Sheria hizi zinakataza na kukemea aina zote za ubaguzi kwa misingi ya; rangi, kabila, ulemavu na kadhalika. Sera ya Taifa ya ulemavu inabainisha hali ya ulemavu kuwa ni, βkutokuwa au kupungukiwa na uwezo wa kushiriki kwa usawa katika shughuli za kawaida za kijamii kutokana na sababu za mapungufu ya kimwili, akili au kijamiiβ. Sera hii inatoa mwongozo wa kutolewa kwa haki na fursa sawa kwa walemavu kupata mambo na huduma za msingi kama; elimu, taarifa, ajira, matunzo, huduma za afya, kumudu na kufikia huduma muhimu. Katika siku za karibuni kumeongezeka vitendo vya kikatili dhidi ya Albino ambavyo ni pamoja na mauaji ya kikatili na kukatwa viungo kutokana na imani za kishirikina. Watu wenye ualbino wanalindwa kisheria kutokana na vitendo hivi kwa kupitia sheria zilizopo za makosa ya jinai.
Serikali pia imechukua hatua za kudhibiti hali hii isiendelee kutokea ikiwa ni pamoja na kuanza kuwaandikisha rasmi (kufanya sensa) watu wenye ualbino, na pia kuanzishwa kwa ulinzi kwa Albino kupitia jeshi la polisi na jamii kwa ujumla, kwa mfano; watoto Albino wanapokwenda shule. Suala la Albino limeendelea kupewa umuhimu mkubwa kitaifa, ikiwa ni pamoja na mjadala wa kitaifa. Mfano; ujumbe wa mbio za Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2009 ulilenga kuhamasisha jamii kuhusu mauaji na vitendo vya kikatili dhidi ya Albino. Mauaji na vitendo vya kikatili dhidi ya Albino vinavyotokea sasa hivi pia vimepelekea serikali kuchukua hatua na kuongeza ulinzi ili kulinda haki za Albino kwa mfano; zimeundwa mahakama maalumu za kusikiliza makosa hayo ili kuharakisha upatikanaji wa haki kwa wahusika. Mpaka sasa watuhumiwa saba wa mauaji ya Albino wamekutwa na hatia na kuhukumiwa kifo kwa kunyongwa.
Je, mtu anaweza kuzuia kupata mimba baada yakujamiiana bila kinga (kufanya ngono zembe) kwa mfano amebakwa?
Updated at: 2024-05-25 16:24:09 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kama umebakwa au kulazimishwa kujamiiana unaweza kupata huduma katika hospitali, kituo cha afya , zahanati au kutoka kwa mhudumu wa afya ambaye atakupatia vidonge vya dharura vya kuzuia mimba. Hivi ni vidonge ambavyo vinatumika ili kupunguza uwezekano wa kupata mimba kama ulijamiiana bila kinga, au umesahau kutumia njia yako ya uzazi wa mpango au ulilazimishwa kujamiiana.
Ili ufanye kazi, njia hii ya dharura ya kuzuia mimba inatakiwa itumiwe ndani ya saa 120 (ndani ya siku tano) baada ya tukio. Inakuwa vizuri zaidi kama njia hii ya dharura itatumika punde bila kusubiri kwani kwa kufanya hivyo, ufanisi wake unakuwa wa kuaminika zaidi.
Hii njia ya dharura inazuia tu mimba kutungwa, haiwezi kusababisha kutoka kwa mimba pindi mimba ikishatunga. Utakapotafuta msaada wa kupata huduma ya vidonge vya dharura vya kuzuia mimba hasa kwa wale waliobakwa au kulazimishwa , mwombe mhudumu akusaidie kupata huduma ya kuzuia maambukizo ya UKIMWI. (Post exposure prophylasis). Unaweza kupata taarifa zaidi kwa mtoa huduma wa uzazi wa mpango kwenye kliniki za serikali, kliniki za UMATI, kliniki za Marie Stopes au sehemu yoyote wanapotoa njia za kisasa za uzazi wa mpango.