Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/right_sidebar.php on line 13

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/right_sidebar.php on line 13
Sidebar with Floating Button
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 3

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 14

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 14
MHUBIRI
☰
AckyShine
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line 4

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Featured Image

Rozari ya Bikira Maria
Mwongozo wa namna ya Kusali Rozari Takatifu ya Mama Bikira Maria




Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema β€œKwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.





Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, β€œTusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).





Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.





Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika:
β€œMungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”





Au;





β€œUtuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..” Au;
β€œSalamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.





Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi.
Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.





Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.





Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Maria…, β€œAtukuzwe..”, β€œEe Yesu wangu…” na β€œTuwasifu milele…” kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.





MATENDO YA ROZARI TAKATIFU





MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)





Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.





Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.





Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara





Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.





Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.





MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)





Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.





Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.





Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.





Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.





Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.





MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)





Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.





Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.





Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.





Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.





Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.





MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)





Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.





Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.





Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.





Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.





Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.





LITANIA YA BIKIRA MARIA





  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utusikie
  • Kristo utusikilize




  • Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
  • Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
  • Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
  • Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie




  • Maria Mtakatifu ………. utuombee
  • Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
  • Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee




  • Mama wa Kristo ……… utuombee
  • Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
  • Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
  • Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
  • Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
  • Mama usiye na doa ……….. utuombee
  • Mama mpendelevu ………. utuombee
  • Mama mstajabivu ………. utuombee
  • Mama wa Muumba ………. utuombee
  • Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
  • Mama wa Kanisa……….. utuombee




  • Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
  • Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
  • Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
  • Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
  • Bikra mweye huruma ………….. utuombee
  • Bikra mwaminifu………….. utuombee




  • Kioo cha haki ………….. utuombee
  • Kikao cha hekima ………….. utuombee
  • Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
  • Chombo cha neema ………….. utuombee
  • Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
  • Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
  • Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
  • Mnara wa Daudi ………….. utuombee
  • Mnara wa pembe ………….. utuombee
  • Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
  • Sanduku la Agano ………….. utuombee




  • Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
  • Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
  • Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
  • Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
  • Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
  • Msaada wa waKristo ………….. utuombee




  • Malkia wa Malaika ………….. utuombee
  • Malkia wa Mababu ………….. utuombee
  • Malkia wa Manabii ………….. utuombee
  • Malkia wa Mitume ………….. utuombee
  • Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
  • Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
  • Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
  • Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
  • Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
  • Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
  • Malkia wa amani ………….. utuombee









  • Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
  • Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
  • Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.









  • Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.




Tuombe





Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.









Karibu Vitatabu vya Kikatoliki









[products orderby="rand" columns="4" category="vitabu-vya-dini" limit="20"]
AckySHINE Solutions

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line 4

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

James Malima (Guest) on October 24, 2018

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Ruth Mtangi (Guest) on October 3, 2018

Imani inaweza kusogeza milima

Stephen Mushi (Guest) on July 25, 2018

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Esther Cheruiyot (Guest) on May 27, 2018

Amina

Lucy Mahiga (Guest) on April 9, 2018

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Maimuna (Guest) on February 12, 2018

πŸ™πŸ™πŸ™

Frank Sokoine (Guest) on December 22, 2017

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

David Nyerere (Guest) on July 19, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Irene Makena (Guest) on June 5, 2017

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Catherine Mkumbo (Guest) on April 29, 2017

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Lydia Mutheu (Guest) on March 4, 2017

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Daniel Obura (Guest) on October 3, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Jane Muthoni (Guest) on October 1, 2016

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Raphael Okoth (Guest) on September 22, 2016

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Lydia Wanyama (Guest) on September 20, 2016

Tembea kwa imani, si kwa kuona

James Kimani (Guest) on July 11, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Esther Nyambura (Guest) on April 18, 2016

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Violet Mumo (Guest) on February 27, 2016

Neema ya Mungu inatosha kwako

James Malima (Guest) on January 27, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Alice Wanjiru (Guest) on December 29, 2015

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Anna Malela (Guest) on December 22, 2015

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Fredrick Mutiso (Guest) on November 1, 2015

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Thomas Mwakalindile (Guest) on October 21, 2015

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Joy Wacera (Guest) on September 30, 2015

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Paul Ndomba (Guest) on April 11, 2015

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Related Posts

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia ... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa... Read More

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kut... Read More

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie ... Read More

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.

Kwenye Msalaba Sali:

... Read More
KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

SALA YA MATUMAINI

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu,

natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,

neema zako duniani na ... Read More


Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_36018e79a10afbaeeb39bac21961ad44, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/bottom_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/bottom_menu.php on line 3
πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact