Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_7ae2ed11fc12a91a4cb90a02801d685a, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga
Date: May 30, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Biriani ni miongoni mwa vyakula ambavyo ni nadra sana kupikwa katika familia nyingi tofauti na vyakula vingine. Inawezekana ni kutokana na watu wengi kutoelewa namna ya kuoika chakula hiki kutokana na kuhitaji viungo vingi ambavyo huwapa usumbufu wapishi.
Kuna aina mbalimbali za upishi wa biriani ambapo mara nyingi hutofautiana kutokana na viungo vinavyotumika katika upishi.
Biriani la mbogamboga ni miongoni mwa aina hizo za upishi. Chakula hiki kinaweza kuliwa na kila mtu hususan wale wasiotumia nyama wala samaki.
Mahitaji:
Β½ kg mchele wa basmati
Kitunguu maji kikubwa 1
Nyanya 1 kubwa
Karoti 1 kubwa
Njegere robo kikombe
Kiazi ulaya 1 kikubwa
Tangawizi za kusaga kijiko 1
Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1
Karafuu kijiko 1
Majani ya kotimili fungu 1
Maziwa ya mtingi ΒΌ kikombe
Chumvi na pilipili kiasi
Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani
Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani
Mafua ΒΌ lita
Maandalizi:
Chemsha mchele na kisha weka pembeni
Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya
Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja
Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri
Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania
Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo
Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30
Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_7ae2ed11fc12a91a4cb90a02801d685a, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
MAHITAJI
Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) - vikombe 2
...
Read More
Mahitaji
Mchele (rice 1/2 kilo)
Mchicha uliokatwakatwa (spinach mafungu 2)
Nyam...
Read More
Mahitaji
Mchele - 2 Mugs
Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg) - Mug
Tuna...
Read More
Nini maana ya lishe?
β’ Lishe yahusu mafunzo ya chakula na jinsi miili ...
Read More
MAHITAJI
Unga - 1 Kikombe
Sukari ya kusaga - 3/4 Kikombe
Siagi - 125 gms
<...
Read More
Mahitaji
Mackerel 2
Kitunguu swaum na tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko c...
Read More
Mahitaji
Mchele wa biriani - 5 gilasi
Nyama ya ngombe ya mifupa - 1 Β½ kilo na nusu...
Read More
Viambaupishi
Mchele 3 vikombe
Nyama ya kusaga 1 LB
Mchanganyiko wa Nafaka (up...
Read More
Vipimo
Mrowanishe kuku na viungo hivi kwa muda mdogo tu
Kuku (Mkate kate Vipande) -...
Read More
Karibu tena jikoni, leo tunaandaa vitafunwa kwa ajili ya kifungua kinywa asubuhi.
Njia za kupima Afya
Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;
Read More
Viamba upishi
Maziwa ya unga 2 vikombe
Sukari 3 vikombe
Maji 3 vikombe
...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!